Blogger Widgets
Home » , » PHOTO | KILI MUSIC TOUR - Ilivyokuwa Kahama

PHOTO | KILI MUSIC TOUR - Ilivyokuwa Kahama


  Kwa mara ya kwanza katika historia ya mji wa Kahama na vitongoji vyake, wakazi wake walipata nafasi ya kuwashuhudia wakali wa muziki zaidi ya 10 katika jukwaa moja katika tamasha la Kilimanjaro Music Tour 2013 lililofanyika katika uwanja wa taiga Kahama na kushuhudiwa na maelfu ya wakazi wa rika zote waliojitokeza na kuujaza uwanja wote.  Wakali hao Linex, Profesa Jay, Roma, Ben Pol, Fid. Q, Lady Jaydee, Izzo Bizness, Barnaba na Recho walilishambulia jukwaa kwa masaa sita mfululizo huku wakati mmoja wakipata nafasi ya kumuimbia Ben Pol wimbo wa Birthday kutokana na kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa usiku wa kuamkia Jumapili.
 Linex akilishambulia jukwaa na wimbo wake wa Aifola
 Recho na madansa wake katika steji ya Kili Music Tour Kahama
 Shabiki mmoja alipata nafasi ya kucheza na Recho
 Kutoka backstage: Izzo Bizness, Alice, Fid Q, Kala Jeremiah na Ben Pol
 Ben Pol na Alice wakiimba wimbo wao mpya wa Waubani
 Ben Pol akiwaimbisha mashabiki kwa hisia
 Barnaba Boy jukwaani
 Linex katika backstage ya Kili Music Tour
 Izzo Bishara, Izzo Bizness akiiwakilisha Mbeya mjini Kahama
 Izzo Bizness na Barnaba wakishambulia jukwaa kwa pamoja
 Baada ya kushuka jukwaani mashabiki hawakutaka kupoteza nafasi ya kupiga nae picha.
 Othman Michuzi na wadau wengine wa Kili wakiteta jambo
 Hip Hop ikiendelea kuwakilishwa na Kala Jeremiah
 Kala Jeremiah akiwauliza mashabiki kama wameilewa Kikwetu kwetu
 Jibu la mashabiki lilikuwa ni hili
Roma Mkatoliki akiwarusha mashabiki waliofurika uwanja wa taifa Kahama
 Ma-DJ kazini kuhakikisha hakuna kinachoharibika
 Linex akiwa na wadau Shaaban Mpondela na Pius toka Frontline Novelli
 Lady Jaydee na Profesa Jay wakiimba Joto Hasira
 Profesa Jay akiifunga Kili Music Tour Kahama
Mashabiki wakinyoosha mikono juu kuwashukuru wakali wa muziki waliopanda jukwaani
© Dvj Sweetp Dj | Radio Producer | Sales and Marketing | Social Media Admin For hire +255 753 672 877

0 comments:

Post a Comment

.