Blogger Widgets
Home » , » Habari | "Tutarudisha Kodi yote ya Sharo Millionea"

Habari | "Tutarudisha Kodi yote ya Sharo Millionea"


WAMILIKI wa nyumba aliyokuwa akiishi msanii wa Komedi, Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’ wamesema watarudisha kiasi chote cha fedha ya kodi ya pango kilichotolewa na nyota huyo. Wakiongea na Saluti5 jana, wamiliki hao wameahidi kukabidhi pesa zote za kodi ya pango zilizokuwa zimelipwa na Sharo, siku vitakapokuwa vinatolewa vyombo.
“Hatuwezi kuzuia hela iliyotolewa na Sharo kama kodi ya pango kwa sababu kitendo hicho ni sawa na dhuluma ambayo ni kosa kwa mujibu wa dini yetu ya Kikristo,” walisema wamiliki hao.
Walisema kuwa, watairudisha kodi hiyo kwasababu Sharo alihamia kwenye nyumba yao takriban wiki moja tu kabla ya ajali iliyosababisha mauti kumfika.
Nyumba aliyoishi Sharo kwa wiki moja tu maeneo ya Sinza B, Dar es Salaam


Sehemu nyumba aliyokuwa akiishi Sharo, Sinza B, geti jeusi ndio la kuingilia kwenda kwenye nyumba ya ndani aliyopanga msanii huyo.
Hii ndio nyumba ya kina Sharo Milionea ya kule Lusanga, Muheza
Chanzo:www.saluti5.com

© Sweetbert Philemon This Is HABARI™

0 comments:

Post a Comment

.